Header Ads

Header ADS

WHO yasema ni mapema kuongelea mwisho wa corona

 


Mkurugenzi wa Programu ya Hali ya Dharura ya Shirika la Afya Ulimwenguni Mike Ryan amesema kuwa sio kweli kutarajia  kumalizika kwa virusi vya corona mwisho wa mwaka.

Mkurugenzi Mkuu wa (WHO) Tedros Adhanom Ghebreyesus amefanya mkutano wa video kwenye makao makuu ya shirika huko Geneva, Uswizi.


Ghebreyesus amesema kuwa kesi za (Kovid-19) zimeongezeka kwa mara ya kwanza wiki iliyopita baada ya kupungua kwa wiki 7.


Mike Ryan, Mkurugenzi wa Programu ya Hali ya Dharura ya WHO, pia amesema,


"Ni mapema mno kuongelea kumalizika kwa janga mwishoni mwa mwaka wa 2021. Sio kweli.".


Akisisitiza kuwa WHO inazingatia kuzuia kuenea kwa virusi, Ryan alisema,


"Suala ni kwamba tunaweza kudhibiti virusi lakini kwa sasa vimezidi."



No comments

Powered by Blogger.