Header Ads

Header ADS

Padre aliyewanyanyasa watoto kingono afia gerezani

 


Padri wa zamani wa Kanisa Katoliki ambaye alifungwa jela kwa kuwanyanyasa kingono watoto watatu pamoja na mwanafunzi aliyekuwa akisomea upadri amefariki jela.

Paul Moore, ambaye alikuwa na umbri wa miaka, alitekeleza uhalifu huo katika maeneo tofauti mjini Ayrshire kati ya mwaka 1977 na 1996.


Alifungwa miaka tisa jela kufuatia uchunguzi wa BBC, lakini kifungo hicho kilipunguzwa hadi miaka minane na majaji wa mahakama ya rufaa.


Uhalifu wa Moore ulichukua zaidi ya miaka 20 kujulikana na mmoja wa wahasiriwa alikuwa na miaka mitano.


Msemaji wa Dayosisi ya Galloway alisema: “Askofu Nolan ataombea roho ya Paul Moore msamaha na amani kwa wale walioteseka katakana na kitendo chake.



No comments

Powered by Blogger.