Header Ads

Header ADS

Unadhani Lulu Anatakiwa Kumfanyia nini Mama Kanumba ili Wote Waishi kwa Amani na Furaha?

 Kwa mtazamo wako je ni sahihi au sio sahihi baadhi ya waandishi kuendelea kumfuata Mama Kanumba kumhoji kuhusu kifo cha Kanumba ilihali Lulu alishahukumiwa kutumikia kifungo na kutoka kwa kwa mujibu wa taratibu za kiserikali?


Kwa mtazamo wako je Lulu hajutii au kuumizwa na tukio hilo la kifo cha Kanumba?


Lulu na Mama yake walijaribu kuwa karibu na Mama Kanumba watu waliona mapichapicha yao Hadi videos wakiwa pamoja kwa furaha Kisha kufarakana



Kuna nyakati Mama Kanumba takribani Mara mbili alisema kasemehe na kumuachia Mungu lakini baadaye anaibuka tena kuonesha hajasamehe


Tunaambiwa Mama Kanumba alipata pole ya pesa nyingi Kisha kununua nyumba hapa dar, na kampuni ya Kanumba ilikuwa bado inafanya kazi na aliacha vifaa, je Mama Kanumba aliviuza au Kama anavyo imeshindikana kukodisha


tunajua sote aliyefariki hawezi kurudi Tena, Mama Kanumba pia alimpoteza Seth


Lakini kwa mtazamo wako wewe unadhani kipi kifanyike ili kuyamaliza Mama Kanumba akubali yaliyotokea kuwa yashatokea , aikubali hali Kama wazazi wengine ambao wamefiwa na watoto kwa namna Kama ya Kanumba


Unadhani Lulu anatakiwa kumfanyia nini Mama Kanumba ili wote waishi kwa amani na furaha?



No comments

Powered by Blogger.