Header Ads

Header ADS

Treni ya Mwendo Kasi Dar Moro Kuanza Kutumika Mwaka Huuu

Ujenzi wa Reli ya Kisasa ya Umeme (SGR) kipande cha kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro, kinatarajiwa kukamilika na kuanza kutumika mwaka huu, baada ya Serikali kutoa Tsh. 274 Bilioni


Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas amesema ni treni ya kisasa na ya kasi kuliko zote ukanda wa Afrika. Ameeleza kuwa, kuna mataifa mengine yamejitahidi kuwa na Treni zinazoenda Kilomita 120 kwa saa, akifafanua ya Tanzania itakwenda Kilomita 160 kwa saa


Dkt. Abbas amesema atatoa ratiba ya siku ambayo kutakuwa na majaribio kwa mara ya kwanza katika Reli ya mwendo kasi, na atatoa tarehe ambayo vichwa vya kisasa vya treni vitapokelewa



No comments

Powered by Blogger.