Header Ads

Header ADS

Ginimbi Kadungure : 'Nataka kila mtu atakayeudhuria mazishi yangu avae nguo nyeupe'

 


Familia ya milionea maarufu nchini Zimbabwe, Ginimbi Genius Kadungure - aliyefariki na ajali ya gari Novemba 8, inasema watu watakaoudhuria mazishi ya milionea huyo siku ya Jumamosi lazima wavaa nguo nyeupe.


Mavazi hayo meupe yatavaliwa kama sawa na wakati alipokuwa hai, aliandaa sherehe na kutaka kila mmoja apendeze kwa kuvaa nguo nyeupe.


Vilevile alikuwa anawakumbusha mara nyingi kuwa hivyo ndivyo angependa kuzikwa , watu wasiwe na haraka haraka ya kumzika na wavae nguo nyeupe katika mazishi yake.


"Mchukue muda kupanga mazishi yangu. Nitahitaji kila anayehudhuria mazishi yangu avae nguo nyeupe tu, kupendeza ni lazima siku hiyo.


Tafadhali kumbuka kuchukua muda wenu muwezavyo kupanga mazishi yangu. Kumbuka ,nitakuwa nimevalia nyeupe tu. Hicho tu ndio ninakihitaji kwenye mazishi yangu." Juliet ambaye ni dada yake alinukuu maneno ya kaka yake alivyosisitiza kabla ya kifo chake.


Ginimbi Genius Kadungure, alifariki siku ya Jumapili , majira ya asubuhi katika mji wa Borrowdale, Harare, Zimbabwe.


Jina lake halisi ni Genius Kadungure na alikuwa maarufu kwa jina la Ginimbi.


Aizaliwa Oktoba 10,mwaka 1984. Hivyo amefariki akiwa na miaka 36.


Alikuwa mfanyabiashara maarufu , alikuwa mwenyekiti wa kampuni ya Piko Trading Holdings & Founder of Genius Foundation, na mmiliki wa klabu ya Sankayi (AKA Dreams Nightlife Club).


Alikuwa na 'Master of Business Administration - alipata MBA yake katika chuo kikuu cha at Great Zimbabwe.


Aliishi: Govan Mbeki, Mpumalanga, Afrika Kusini ingawa nyumbani ni Harare, Zimbabwe.



Mlimbwende huyu alikuwa maarufu Zimbabwe, alifariki akiwa kwenye gari moja na milionea Ginimbi Genius Kadungure.


Jina lake kamili ni Michelle Moana Amuli,.


Ripoti zinasema kulikuwa na zaidi ya abiria mmoja na wote walifariki ndani ya gari lililopata ajali baada ya gari hilo kuwaka moto.


Kwa mujib wa ripoti ya polisi, Ginimbi, Moana na abiria wengine wawili walikuwa wametoka kwenye sherehe ya kumbukumbu ya kuzaliwa ya Moana aliyekuwa anatiiza miaka 26.


Kwa mujibu wa iHarere News, abiria wengine wawili ni Rolls Royce Wraith na Limumba Karim - mmoja akiwa raia wa Malawi na mwingine raia wa Msumbiji alifahamika kama 'Elisha'.




No comments

Powered by Blogger.