Header Ads

Header ADS

Tahadhari kwa Wazazi Wanaogiza Wasichana wa Kazi Toka Mikoani ,Ambao Unatoa Pesa na Kutumiwa Mdada wa Kazi

Nimepokea huu ujumbe kutoka Arusha..Nami nimeona si vibaya na wewe ukausoma;

Onyo kwa wazazi wanaogiza wasichana wa kazi,ambao unatoa pesa unatumiwa! Jana huko Arusha ilikuwa hivi;

Mschana wa kazi alitoroka na mtoto wa miaka kumi tangu saa kumi usiku akamuacha wa miaka 5 akamwambia tunakuja,mtoto mdogo wa miaka 5 aliogopa chumbani na kuamua kwenda kugonga kwa mama yake, kuanzia saa kumi usiku dada hakujulikana alipo na mtoto wa miaka 10, mama alitangaza Redio Safina na Monchwary alienda hola! Kamanda wa polis na jeshi la polis jana walitanda mji wa Arusha na kukagua kila gari bila mafanikio, Baadae sana wakaona Tax nyeusi wakasimamisha dada kabadili mavazi na mtoto wa miaka 10 akiwa amelala tu gari ikawapelekwa kituo cha polisi kusachia dada kakutwa na kisu kipya kikali sana, anaulizwa alikuwa wanaenda wapi hajibu, kisu cha nini nilikuwa naenda kumuuwa mimi huwa nafanyaga hivyo na hii sio mara moja hii ni kazi yangu cha ajabu yule mtoto mpaka saa 6 tunapigiwa simu ajazinduka, hasemi kampa nini mtoto, mtoto amepelekwa hospitali kwa uchunguzi,wazaz wezangu watoto wetu tunawapata kwa shida sana katika kujifungua tuwe makini uzazi umekuwa mgumu sana na hao wasichana wakutumiwa katika gari mh mh!! Msichana wa kirangi anajibu mimi ndio kazi yangu nishawauwa wengi sana bila kuogopa police inatisha...


No comments

Powered by Blogger.