Header Ads

Header ADS

Kisa Manula, Shabiki Apigwa Faini ya Elfu 20 Simba



KATIKA hali isiyotarajiwa, kwenye mazoezi ya Simba, kocha mpya wa makipa wa timu hiyo raia wa Afrika Kusini, Tyron Damos, alimkamata shabiki mmoja akirekodi mazoezi aliyokuwa akimpa kipa wake Aishi Manula na kuamuru shabiki huyo alipe faini ya Sh 20,000.


Kwenye mazoezi hayo yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Simba MO arena, Bunju Dar es Salaam, Simba waliruhusu watu mbalimbali kurekodi mazoezi hayo kwa dakika 15 tu kabla ya kuzuia kurekodi
mazoezi ya kimbinu.

 


Licha ya zuio hilo shabiki mmoja aliendelea kurekodi na kumfanya kocha huyo Msauzi kumshtukia ambapo
alisimamisha mazoezi na kumfuata shabiki huyo na kumwambia anapaswa kulipa faini ya Sh 20,000 kwa kukiuka maelekezo.




Championi Ijumaa, lililokuwa uwanjani hapo lilishuhudia kocha Tyron akisema: “Nimekuona ulikuwa ukirekodi programu zetu za kiufundi nilizokuwa nampa Manula na kwa kuwa hiyo ni kinyume cha maelekezo basi utapaswa ulipe faini ya shilingi 20,000.”


Mwishoni kocha huyo alianza kutabasamu na kumwambia shabiki aliyekuwa akirekodi kuwa alikuwa anamtania, na kumtahadharisha kuwa asiendelee kufanya hivyo.

 
STORI: JOEL THOMAS,Dar es Salaam


No comments

Powered by Blogger.