Header Ads

Header ADS

Davido Kuanza Mwaka na Collabo Kubwa na Drake, Athibitisha Kwa Kupigiana Video Call


Mwanamuziki nyota kutoka Nigeria @davido amethibitisha uwepo /ujio wa collabo yake na rapper kutoka canada #Drake mwakani 2022.

Kupitia insta story yake Davido ameshare sehemu ya video akiwa anazungumza na rapper huyo kupitia video call na kusindikiza na ujumbe unao ashiria uwepo wa collabo baina yao ifikapo mwaka 2022.

Kama collabo hiyo itafanikiwa basi Davido atakua msanii wa pili mkubwa kutoka Nigeria kufanya kazi na #Drake ,nyuma ya #WizKid ambae tayari amekwisha fanya nae kazi miaka kadhaa nyuma kwenye nyimbo kama 'Closer & One dance'



No comments

Powered by Blogger.