Header Ads

Header ADS

Tanzia: Nyota Mtibwa Sugar Afariki




MADILU Mosha, aliyekuwa mchezaji wa Klabu ya Vijana ya Mtibwa Sugar ya Morogoro ametangulia mbele za haki.

 

Taarifa rasmi iliyotolewa na Mtibwa Sugar kupitia Ukurasa rasmi wa Instagarm leo Agosti 3, 2021 imeeleza:”Timu ya Mtibwa Sugar pamoja na uongozi wake umepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha aliyekuwa mchezaji wa timu ya vijana Madilu Mosha.

 

“Tunaungana na familia, ndugu, jamaa na marafiki katika kipindi hiki kigumu. Tunaomba Mungu awape subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu na ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi, Ameen,”.

Pumzika kwa amani mwanafamilia ya michezo.


No comments

Powered by Blogger.