Header Ads

Header ADS

Mhasibu mkuu wa kampuni ya Donald Trump afunguliwa mashtaka kwa udanganyifu wa ushuru Marekani

 


Kesi ilifunguliwa dhidi ya kampuni ya Rais wa zamani wa Marekani Donald Trump na afisa wake mkuu wa uhasibu (CFO), Allen Weisselberg, kwa mashtaka 15 tofauti, pamoja na kughushi rekodi za biashara, ulaghai, na udanganyifu wa ushuru.

CFO Weisselberg wa Trump, ambaye alifikishwa mbele ya mahakama kwa mara ya kwanza hapo jana, alishtakiwa kwa kupokea zaidi ya dola milioni 1.7 kwa fidia isiyosajiliwa, pamoja na kodi ya nyumba, malipo ya gari na ada ya shule.


Kama matokeo ya uchunguzi wa miaka 2, Ofisi ya Mwanasheria wa Manhattan ilisema kwamba kampuni ya Trump na CFO wake Weisselberg, wamehusika katika udanganyifu wa ushuru wa serikali na miji tangu mwaka 2005.


Wakati mashtaka hayakujumuisha kesi yoyote dhidi ya Trump, mawakili wa kampuni ya Trump na Weisselberg, ambao walifikishwa kortini wakiwa wamefungwa pingu, walikana mashtaka dhidi yao.


Weisselberg, ambaye aliulizwa kutoa pasipoti yake kwa sababu alikuwa katika hatari ya kutoroka, aliachiliwa mwishoni mwa usikilizaji ili kuendelea na kesi yake.



No comments

Powered by Blogger.