Header Ads

Header ADS

“Kumchamba MTU Mtandaoni ni Kosa Kisheria” Waziri Ndugulile



Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile amewataka watu kutumia Mitandao ya Kijamii vizuri na kuepuka makosa ya mtandaoni.

Dk. Ngugulile ameyasema hayo  jijini Dodoma  katika uzinduzi wa tovuti ya wizara hiyo pamoja na mpango mkakati wa 2021/26.

Waziri amebainisha kuwa ukatumia ukurasa wa Instagram kumsema mtu vibaya ‘kumchamba’ ni kosa kisheria au kumkashifu mtu mtandaoni ni kosa hata kama mtu atatumia jina lisilo halisi katika TEHAMA akitenda uhalifu atabainika na kuchukuliwa hatua.



No comments

Powered by Blogger.