Header Ads

Header ADS

Waziri Ummy: Walimu Wanaojitolea Kuna Barua Feki





Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu amesema yapo malalamiko kuwa baadhi ya Walimu wanaojitolea wanawasilisha barua feki zinazosema wanafanya hivyo wakati hawajitolei.

 

Ametoa kauli hiyo leo Mei 25, 2021 Bungeni Dodoma wakati akimjibu Mbunge wa Longido aliyehoji ni kwanini Seikali isiajiri Walimu ambao wanajitolea.

 

Amesema hata Wanaojitolea watafanyiwa uchambuzi ili kuona kama ni kweli wanafanya hivyo akiongeza, kigezo kikubwa kitakachotumika katika utoaji wa Ajira ni hicho.

 

Ameeleza, suala hilo ni tete ambapo nafasi ni 6,949 ilihali mpaka Mei 23, 2021 walioomba ni 89,958. Ameomba Serikali iaminiwe akisisitiza Haki itatendeka




No comments

Powered by Blogger.