Header Ads

Header ADS

Maiti yazuiliwa hospitali kisa 'Hitilafu ya pasipoti'





Mwanamke ambaye baba yake wa kambo alifariki Thailand wiki mbili zilizopita anasema hospitali imekataa kuachilia maiti yake kutokana na mchanganyiko wa nambari katika pasipoti yake.
Mwili wa David Donoghue, 75, ambaye alihamia Mkoa wa Phuket miaka 15 iliyopita, utachomwa pamoja na miili mingine katika hospitali hiyo siku ya Jumatano ikiwa dosari hiyo haitarekebishwa.

Gemma Swift amesema kuwa "anawasihi" wafanyakazi wa ubalozi nchini Thailand kushughulikia dosari hiyo anayosema ni "suala la kiutawala"

Ofisi ya mambo ya nje imesema maafisa wake wanajaribu kushughulikia suala hilo ili nyaraka sahihi zipatikane.

Bw. Donoghue, ambaye alikuwa akiishi Bury eneo la Manchester kabla ya kuhamia Thailand, aliugua maradhi ya mapafu.

Alipelekwa hospitali nchini humo kwa ambulensi lakini alikuwa na pasipoti ambayo muda wake wa matumizi umemalizika.

Bi Swift, mkazi wa Abergele, kaunti wa Conwy, anasema Bw. Donoghue alifariki hospitali Februari 15.


No comments

Powered by Blogger.