Header Ads

Header ADS

Kampuni Inayonunua Mkojo Kuchunguzwa

 



Dar es Salaam. Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) imesema haiitambui wala haijawahi kuipatia usajili kampuni ya Polai (Tz). Co Ltd kukusanya mikojo ya wajawazito, kwa maelezo kwamba wanaitumia kutengeneza tiba ya magonjwa ya binadamu.


TMDA imesema kuwa imeshatoa maelekezo kwa meneja wa mamlaka hiyo kanda ya mashariki kuanza mara moja kuifuatilia kwa ukaribu kampuni hiyo na pindi uchunguzi ukikamilika na kuthibitisha makosa yao, watatoa taarifa kwa umma kuhusu hatua watakazochukua kwa mujibu wa sheria.


Hivi karibuni gazeti hili liliripoti habari ya uchunguzi wa siku 14 uliobaini kuwa ukusanyaji wa mikojo ya wajawazito unafanyika kwa usiri mkubwa jijini hapa, kwa wajawazito hao ambao kufuatwa majumbani na kushawishiwa kukubali.



No comments

Powered by Blogger.