Header Ads

Header ADS

Baada ya Kukosa Ushindi Mbele ya Simba, Al Merrikh Yamtimua Kocha Wake

 


Muda mfupi baada ya kutoka sare tasa na Simba leo nyumbani huko Sudan, Al Merrikh imemfukuza kocha wake Nasreddin Nabi na Benchi lake lote la ufundi


Nabi ametimuliwa akiwa ameiongoza timu hiyo kwa siku 34 tu tangu alipojiunga nayo Februari 2 mwaka huu akichukua mikoba ya Mserbia Midrag Jesic


Matokeo hayo ya sare yameiweka Al Merrikh katika nafasi ngumu ya kufuzu hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu


Ili ifuzu robo fainali, inahitajika kuibuka na ushindi katika mechi zake zote tatu zilizobakia za mzunguko wa pili dhidi ya Simba, Al Ahly na AS Vita Club.



No comments

Powered by Blogger.