Header Ads

Header ADS

Rap Lil Uzi Vert amekua gumzo baada ya kuweka Almasi ya bilioni 55.4 kwenye paji la uso






Nyota wa Muziki wa Rap Lil Uzi Vert  amezua gumzo na kuwashangaza watu wengi baada ya kuamua kuweka Almasi iliyogharimu mpunga mrefu kwa ajili ya kupendezesha Paji lake ka uso,
Rapa huyo ametumia dolla million 24 (Takribani Bilioni 55.4 za Kitanzania) kuweka almasi hiyo yenye rangi ya Pinki kama urembo, #LilUziVert, amedai haikuwa rahisi kufanikisha jambo hilo kwani ilimbidi kuanza kulipia pesa kidogo kidogo tangu mwaka 2017 kwa ajili ya mchakato huo,

Almasi hiyo ya imepandikizwa katikati ya paji lake la Uso, Baadhi ya Mashabiki zake hawajafurahishwa na kitendo hicho wakidai huenda kikahatarisha maisha yake ingawa amewatoa hofu kwani tayari ameikatia Bima.



No comments

Powered by Blogger.