Header Ads

Header ADS

Afrika Kusini imeondoa marufuku ya uuzwaji wa pombe




Afrika Kusini imeondoa marufuku ya uuzwaji wa pombe
Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amelegeza masharti dhidi ya virusi vya corona ikiwa ni pamoja na kuruhusu pombe kuanza kuuzwa tena.
Fukwe zitafunguliwa na nyumba za ibada zitafunguliwa kwa kuruhusu idadi ndogo ya watu.

Tangazo hilo limekuja wakati bwana Ramaphosa akifurahia ujio wa chanjo nchini mwake.

Dozi milioni moja za chanjo ya AstraZeneca - zinaweza kubadilisha hali ilivyo ya Covid-19 nchini humo.

Kwa barani Afrika, Afrika Kusini inaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya maambukizi ya corona na vifo vilivyotokana na Covid 19.

Tangu janga la corona lianze, zaidi ya watu milioni 1.4 walipata maambukizi ya virusi vya corona na vifo 44,164 vilivyotokana na janga hilo kwa mujibu wa utafiti wa chuo kikuu cha Johns Hopkins.

Mataifa mengi yameiwekea vikwazo vya usafiri Afrika Kusini kwa kuweka marufuku kwa abiria kutoka taifa hilo kuingia nchini mwao ili kuzuia maambukizi ya wimbi jipya la virusi vya corona ambavyo vinadhaniwa kuwa vimeanzia nchini humo na vinavyoshukiwa kuwa sugu hata kwa chanjo iliyopo.



No comments

Powered by Blogger.