Header Ads

Header ADS

Yanga Yaridhishwa na Kiwango Cha Mukoko, kumuongezea mkataba Kabla Nyakunyaku Ajamnasa

 


 MABOSI wa Yanga wameweka wazi kuwa watamuongezea mkataba kiungo bora ndani ya Ligi Kuu Bara kwa msimu wa 2020/21 kwa mwezi Oktoba, Tonombe Mukoko anayetajwa kuingia anga za Simba.

Ikiwa watamuongeza mkataba nyota huyo watazima ndoto za watani zao wa jadi kuipata saini ya kiungo huyo ambaye ni miongoni mwa wanaofanya vizuri kwa msimu wa 2020/21 na kuingilia kati dili hilo kibabe.


Mukoko aliibuka ndani ya Yanga kwenye dirisha kubwa akitokea Klabu ya AS Vita ya Congo pamoja na mwenzake Tuisila Kisinda ambao kwa pamoja wamekuwa na pacha matata ndani ya uwanja.


Kwa msimu huu pacha yao imekuwa na moto ambapo kwenye Dar Dabi, Kisinda alisababisha penalti iliyofungwa na Michael Sarpong huku Mukoko akisepa na tuzo ya mchezaji bora wa mchezo huo ikiwa ni dabi yao ya kwanza.



No comments

Powered by Blogger.