Header Ads

Header ADS

Hamisa Mobeto Afunguka Kumzalia Watoto Watano Diamond


Wakati ndoa ya staa mkubwa wa muziki barani afrika, Nasibu abdul ‘Diamond Platnumz’ ikinukia, habari mpya ni kwamba mzazi mwenzake, mwanamitindo Hamisa Mobeto, amefunguka kuwa haoni tatizo kumzalia staa huyo mtoto wa tano, Gazeti la IJUMaa linakushushia mchapo kama wote!

ISHU IMEaNZIa INSTAGRAM

Mchongo huu ulianzia kwenye mitandao ya kijamii hususan Instagram ambako kulizagaa tetesi kuwa bwana Nasibu a.k.a Mondi ameshafanya yake kwa Mobeto na ujauzito ukitajwa kuwa na umri wa miezi mitatu.

“Wabongo wanasema bora mtu akunyime chakula, lakini siyo umbeya, kwa taarifa za sasa hivi unaambiwa mambo yameshataradadi huko kwa Mobeto na Chibu (Nasibu) ameshaweka chata nyingine kwa bidada hapa tulipo Dyllan anasubiria mdogo wake…



WAUNGANISHA DOTI…

“Tulikuwa tunajiuliza Hamisa (Mobeto) mbona amechachamaa na Mondi hivi kwenye kumvalisha kumbe mambo ni moto na unaambiwa siku hizi analala kwa Mondi. Ila kinachotushangaza wajameni bibie alisema hawezi kuzaa mtoto mwingine bila ndoa, sasa hatujui imekuwaje,’’ alifunguka mdau mmoja mwenye ushawishi Instagram.



WENGINE WAKAENDA MBALI

Kwenye Instagram, kuna wadau wengine walikwenda mbali zaidi kwa kudai ndiyo maana Mobeto hakuweza kuhudhuria kwenye sherehe ya harusi ya dada wa Diamond, Esma Khan ‘Esma Platinum’ iliyofanyika hivi karibuni kwa sababu Mondi ndiye aliyemzuia kwenda kwani mimba inampeleka puta.



“Wanazengo mnajua kwa nini bimdashi hakutokea kwenye shughuli ya Esma ambaye ni shoga yake wakati kwa Zuchu alikwenda? Unaambiwa mimba inampeleka hovyo anatematema mate mpaka mzee baba (Mondi) akamwambia atulie nyumbani asiende kwenye shughuli hiyo,” aliandika shabiki mwingine anayejiita Mrs–Muhidini.



MOBETO ANASEMAJE?

Ili kujua ukweli juu ya habari hizo Gazeti la IJUMAA lilifanya jitihada za kumpata Mobeto ambapo lilifika nyumbani kwake, Mbezi-Beach jijini Dar, lakini lilimkuta amelala na kushindwa kuzungumza naye ana kwa ana ila baadaye alipatikana kupitia simu ya mkononi.Mazungumzo kati yake (Mobeto) na Gazeti la IJUMAA yalikuwa hivi;

IJUMaa: Mambo

Hamisa,  mzima wewe?

MOBETO: Mimi mzima nani mwenzangu?IJUMaa: Unaongea na mwandishi wa Gazeti la IJUMAA.

MOBETO: Enhe, sema!

IJUMAA: Kuna habari zinasamba kwenye mitandao ya kijamii kuwa una ujauzito wa Mondi na ndiyo maana umekuwa karibu naye kwa kipindi hiki na umekuwa ukimvalisha nguo akiwa anatoka kwenye mambo yake, je, habari hizi zina ukweli kiasi gani?

No comments

Powered by Blogger.