Header Ads

Header ADS

Mnakosea Sana Mahesabu Wadada wa Mjini Kwa Kupenda Watanashati


Mnapenda wanaume wenye pesa, wawe wasafi, wamiliki magari mazuri. Hiyo hesabu ni kama pyramid walio na vitu hivyo ni wachache sana nao kuna waliowasaidia kufikia hapo hawawezi kuwasahau. Inawezekana ni wazazi, ndugu, au wapenzi na wake zao.

Unampenda bank teller anaepata
750,000. Anakatwa student loan, anakatwa mkopo wa vitz, analipa kodi ya chumba na sebule, hajakula wala hajaweka gari mafuta. Unategemea akupe hela ya saloon, akununulie vocha ya simu na kumbom vi 20,000. Unamuongezea pressure, akikukimbia usitafute mchawi.

Wakati kuna mkaka anakaanga chips na mishkaki, anaingiza laki mbili kwa siku na ana uwezo wa kukupa hayo maisha unayotaka. Humtaki kisa status mjini utawaambia nini mashost eti babe mkaanga chips!

Ndiyo hapo mnapokosea hesabu zenu.

No comments

Powered by Blogger.