Header Ads

Header ADS

Wafanyabiashara Simiyu Wakubali Kuuza Sukari 1,900


Wafanyabiashara wa sukari Wilaya ya Bariadi, Mkoa wa Simiyu, wametangaza kushusha bei ya bidhaa hiyo kutoka Sh 3,200 kwa kilo moja ilivyokuwa ikiuzwa awali, hadi Sh 1,900, ili kutii maagizo ya Serikali.


Sukari

Hatua hiyo imekuja kufuatia kikao cha pamoja, baina ya wafanyabiashara wa sukari wa rejareja na jumla na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Festo Kiswaga, kikicholenga kujadili mstakabari wa bei ya bidhaa hiyo.

Katika kikao hicho, Serikali ilisema kuanzia leo Jumanne, itaanza kuwakamata wafanyabiashara watakaobainika kuuza sukari juu ya Sh 1,900, ambayo ni bei elekezi ya mamlaka, na hii ndiyo kauli za Serikali.

No comments

Powered by Blogger.