Header Ads

Header ADS

Iran kuzuia wachunguzi kuvitazama vinu vya nyuklia




Spika wa bunge la Iran amesema leo kuwa huenda wasimamizi wa kimataifa wasipate fursa ya kutazama picha za vinu vya nyuklia vya Jamhuri hiyo ya Kiislamu.

Iran to cold take a look at redesigned spirits reactor – The Balkantimes  Press

Matamshi haya ya Mohammad Bagher Qalibaf huenda yakazidisha mvutano ulioko wakati ambapo juhudi za kidiplomasia zinaendelea mjini Vienna kujaribu kuunusuru mkataba wa nyuklia na nchi zenye nguvu duniani.

Kauli hii ya spika inaashiria jinsi nafasi ya Marekani na nchi zengine zenye nguvu kuafikiana na Iran ilivyo ndogo mno. Iran kwa sasa tayari inaendelea na urutubishaji wa nyuklia kwa viwango vya juu kitu ambacho ni kinyume na makubaliano ya mkataba wa nyuklia wa mwaka 2015.

Source Deutsche Welle




No comments

Powered by Blogger.